___Translations___

_Quran?_

_Gadgets_

_Search_

_Links_

_Contribute_

_Note_

1 - AL-FAATIH'A
2 - AL - BAQARA
3 - AL I'MRAN
4 - AN-NISAAI
5 - AL - MAIDA
6 - AL - AN-A'AM
7 - AL - A'RAAF
8 - AL - ANFAAL
9 - AT-TAWBA
10 - YUNUS
11 - HUD
12 - YUSUF
13 - AR-RAA'D
14 - IBRAHIM
15 - AL - HIJR
16 - AN NAH'L
17 - AL ISRAAI (BANI ISRAIL)
18 - AL - KAHF
19 - MARYAM
20 - T'AHA
21 - AL - ANBIYAA
22 - AL -HAJJ
23 - AL - MUUMINUN
24 - AN - NUR
25 - AL - FURQAN
26 - ASH-SHUA'RAA
27 - AN-NAML
28 - AL-QAS'AS'
29 - AL - A'NKABUT
30 - AR-RUM
31 - LUQMAN
32 - ASSAJDAH
33 - AL-AH'ZAB
34 - SABAA
35 - FAAT'IR
36 - YA-SIN
37 - ASS'AFFAT
38 - S'AAD
39 - AZZUMAR
40 - GHAAFIR (AU AL MUUMIN)
41 - FUSS'ILAT (AU H'A MIM SAJDAH)
42 - ASH-SHUURA
43 - AZZUKHRUF
44 - ADDUKHAN
45 - AL - JAATHIYA
46 - AL - AH'QAAF
47 - MUH'AMMAD
48 - AL FAT-H'I
49 - AL H'UJURAAT
50 - QAAF
51 - ADH-DHAARIYAAT
52 - ATT'UR
53 - ANNAJM
54 - AL-QAMAR
55 - ARRAH'MAN
56 - AL -WAAQIA'H
57 - AL -H'ADIID
58 - AL - MUJAADALAH
59 - AL - H'ASHRI
60 - AL - MUMTAH'INAH
61 - ASS'AF
62 - AL - JUMUA'
63 - AL - MUNAAFIQUN
64 - ATTAGHAABUN
65 - ATT'ALAAQ
66 - ATTAH'RIIM
67 - AL - MULK
68 - AL - QALAM
69 - AL - H'AAQQAH
70 - AL - MAA'RIJ
71 - NUH'
72 - AL - JINN
73 - AL - MUZZAMMIL
74 - AL - MUDDATHTHIR
75 - AL - QIYAMAH
76 - AL - INSAN
77 - AL - MURSALAAT
78 - ANNABAA
79 - ANNAZIA'AT
80 - A'BASA
81 - ATTAKWIR
82 - AL - INFIT'AAR
83 - AL - MUT'AFFIFIIN
84 - AL - INSHIQAAQ
85 - AL - BURUUJ
86 - ATT'AARIQ
87 - AL - AA'LAA
88 - AL - GHAASHIYAH
89 - AL - FAJR
90 - AL - BALAD
91 - ASH-SHAMS
92 - AL - LAYL
93 - WADH-DHUH'AA
94 - ASH-SHARH'
95 - AT-TIN
96 - AL - A'LAQ
97 - AL - QADR
98 - AL - BAYYINAH
99 - AZ-ZILZALAH
100 - AL - A'ADIYAAT
101 - AL - QAARIA'H
102 - AT-TAKAATHUR
103 - AL - A'S'R
104 - AL - HUMAZAH
105 - AL - FIIL
106 - QURAISH
107 - AL - MAAU'N
108 - AL - KAWTHAR
109 - AL - KAFIRUN
110 - ANNAS'R
111 - AL - MASAD
112 - AL - IKHLAS'
113 - AL - FALAQ
114 - ANNAS
KISWAHILI

83 - AL - MUT'AFFIFIIN

 

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.

 
1Ole wao hao wapunjao!
 
2Ambao wanapo jipimia kwa watu hudai watimiziwe.
 
3Na wao wanapo wapimia watu kwa kipimo au mizani hupunguza.
 
4Kwani hawadhani hao kwamba watafufuliwa
 
5Katika Siku iliyo kuu,
 
6Siku watapo msimamia watu Mola Mlezi wa walimwengu wote?
 
7Hasha! Hakika maandiko ya wakosefu bila ya shaka yamo katika Sijjin.
 
8Unajua nini Sijjin?
 
9Kitabu kilicho andikwa.
 
10Ole wao siku hiyo kwa wanao kadhibisha!
 
11Ambao wanaikadhibisha Siku ya Malipo.
 
12Wala haikadhibishi ila kila mwenye kuruka mipaka, mwenye dhambi.
 
13Anapo somewa Aya zetu husema: Ni visa vya watu wa kale!
 
14Hasha! Bali yametia kutu juu ya nyoyo zao hao walio kuwa wakiyachuma.
 
15Hasha! Hakika hao siku hiyo bila ya shaka watazuiliwa na neema za Mola wao Mlezi.
 
16Kisha wataingia Motoni!
 
17Kisha waambiwe: Haya ndiyo mliyo kuwa mkiyakadhabisha.
 
18Hasha! Hakika maandiko ya watu wema bila ya shaka yamo katika I'liyyin.
 
19Na nini kitakacho kujuvya nini I'liyyin?
 
20Kitabu kilicho andikwa.
 
21Wanakishuhudia walio karibishwa.
 
22Hakika watu wema bila ya shaka watakuwa katika neema.
 
23Wakae juu ya viti vya enzi wakiangalia.
 
24Utatambua katika nyuso zao mng'aro wa neema,
 
25Watanyweshwa kinywaji safi kiliyo tiwa muhuri,
 
26Muhuri wake ni miski. Na katika hayo washindanie wenye kushindana.
 
27Na mchanganyiko wake ni Tasniim,
 
28Chemchem watakayo inywa walio kurubishwa.
 
29Kwa hakika wale walio kuwa wakosefu walikuwa wakiwacheka walio amini.
 
30Na wanapo pita karibu yao wakikonyezana.
 
31Na wanapo rudi kwa watu wao hurudi nao wamefurahi.
 
32Na wanapo waona husema: Hakika hawa ndio khasa walio potea.
 
33Na wao hawakutumwa wawe walinzi juu yao.
 
34Basi leo walio amini ndio watawacheka makafiri,
 
35Nao wako juu ya viti vya enzi wakiangalia.
 
36Je! makafiri wamelipwa malipo ya yale waliyo kuwa wakiyatenda?