___Translations___

_Quran?_

_Gadgets_

_Search_

_Links_

_Contribute_

_Note_

1 - AL-FAATIH'A
2 - AL - BAQARA
3 - AL I'MRAN
4 - AN-NISAAI
5 - AL - MAIDA
6 - AL - AN-A'AM
7 - AL - A'RAAF
8 - AL - ANFAAL
9 - AT-TAWBA
10 - YUNUS
11 - HUD
12 - YUSUF
13 - AR-RAA'D
14 - IBRAHIM
15 - AL - HIJR
16 - AN NAH'L
17 - AL ISRAAI (BANI ISRAIL)
18 - AL - KAHF
19 - MARYAM
20 - T'AHA
21 - AL - ANBIYAA
22 - AL -HAJJ
23 - AL - MUUMINUN
24 - AN - NUR
25 - AL - FURQAN
26 - ASH-SHUA'RAA
27 - AN-NAML
28 - AL-QAS'AS'
29 - AL - A'NKABUT
30 - AR-RUM
31 - LUQMAN
32 - ASSAJDAH
33 - AL-AH'ZAB
34 - SABAA
35 - FAAT'IR
36 - YA-SIN
37 - ASS'AFFAT
38 - S'AAD
39 - AZZUMAR
40 - GHAAFIR (AU AL MUUMIN)
41 - FUSS'ILAT (AU H'A MIM SAJDAH)
42 - ASH-SHUURA
43 - AZZUKHRUF
44 - ADDUKHAN
45 - AL - JAATHIYA
46 - AL - AH'QAAF
47 - MUH'AMMAD
48 - AL FAT-H'I
49 - AL H'UJURAAT
50 - QAAF
51 - ADH-DHAARIYAAT
52 - ATT'UR
53 - ANNAJM
54 - AL-QAMAR
55 - ARRAH'MAN
56 - AL -WAAQIA'H
57 - AL -H'ADIID
58 - AL - MUJAADALAH
59 - AL - H'ASHRI
60 - AL - MUMTAH'INAH
61 - ASS'AF
62 - AL - JUMUA'
63 - AL - MUNAAFIQUN
64 - ATTAGHAABUN
65 - ATT'ALAAQ
66 - ATTAH'RIIM
67 - AL - MULK
68 - AL - QALAM
69 - AL - H'AAQQAH
70 - AL - MAA'RIJ
71 - NUH'
72 - AL - JINN
73 - AL - MUZZAMMIL
74 - AL - MUDDATHTHIR
75 - AL - QIYAMAH
76 - AL - INSAN
77 - AL - MURSALAAT
78 - ANNABAA
79 - ANNAZIA'AT
80 - A'BASA
81 - ATTAKWIR
82 - AL - INFIT'AAR
83 - AL - MUT'AFFIFIIN
84 - AL - INSHIQAAQ
85 - AL - BURUUJ
86 - ATT'AARIQ
87 - AL - AA'LAA
88 - AL - GHAASHIYAH
89 - AL - FAJR
90 - AL - BALAD
91 - ASH-SHAMS
92 - AL - LAYL
93 - WADH-DHUH'AA
94 - ASH-SHARH'
95 - AT-TIN
96 - AL - A'LAQ
97 - AL - QADR
98 - AL - BAYYINAH
99 - AZ-ZILZALAH
100 - AL - A'ADIYAAT
101 - AL - QAARIA'H
102 - AT-TAKAATHUR
103 - AL - A'S'R
104 - AL - HUMAZAH
105 - AL - FIIL
106 - QURAISH
107 - AL - MAAU'N
108 - AL - KAWTHAR
109 - AL - KAFIRUN
110 - ANNAS'R
111 - AL - MASAD
112 - AL - IKHLAS'
113 - AL - FALAQ
114 - ANNAS
KISWAHILI

55 - ARRAH'MAN

 

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.

 
1Arrah'man, Mwingi wa Rehema
 
2Amefundisha Qur'ani.
 
3Amemuumba mwanaadamu,
 
4Akamfundisha kubaini.
 
5Jua na mwezi huenda kwa hisabu.
 
6Na mimea yenye kutambaa, na miti, inanyenyekea.
 
7Na mbingu ameziinua, na ameweka mizani,
 
8Ili msidhulumu katika mizani.
 
9Na wekeni mizani kwa haki, wala msipunje katika mizani.
 
10Na ardhi ameiweka kwa ajili ya viumbe.
 
11Humo yamo matunda na mitende yenye mafumba.
 
12Na nafaka zenye makapi, na rehani.
 
13Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
 
14Amemuumba mtu kwa udongo wa kinamo..
 
15Na akawaumba majini kwa ulimi wa moto.
 
16Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
 
17Mola Mlezi wa mashariki mbili na wa magharibi mbili.
 
18Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
 
19Anaziendesha bahari mbili zikutane;
 
20Baina yao kipo kizuizi, zisiingiliane.
 
21Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
 
22Katika hizo bahari mbili zinatoka lulu na marijani.
 
23Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
 
24Na ni vyake Yeye hivi viendavyo baharini vilivyo undwa kama vilima.
 
25Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
 
26Kila kilioko juu yake kitatoweka.
 
27Na atabakia Mwenyewe Mola wako Mlezi Mwenye utukufu na ukarimu.
 
28Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
 
29Vinamwomba Yeye vilivyomo katika mbingu na ardhi. Kila siku Yeye yumo katika mambo.
 
30Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
 
31Tutakuhisabuni enyi makundi mawili.
 
32Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
 
33Enyi makundi ya majini na watu! Mkiweza kupenya kwenye mbingu na ardhi, basi penyeni! Hamtapenya ila kwa kupewa madaraka.
 
34Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
 
35Mtapelekewa muwako wa moto na shaba; wala hamtashinda.
 
36Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
 
37Itakapo pasuka mbingu ikawa nyekundu kama mafuta.
 
38Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
 
39Siku hiyo hataulizwa dhambi zake mtu wala jini.
 
40Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
 
41Watajuulikana wakosefu kwa alama zao, basi watashikwa kwa nywele zao za utosini na kwa miguu.
 
42Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
 
43Hii ndiyo Jahannamu ambayo wakosefu wakiikanusha.
 
44Watakuwa wakizunguka baina ya hiyo na maji ya moto yanayo chemka.
 
45Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
 
46Na mwenye kuogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi atapata Bustani mbili.
 
47Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
 
48Bustani zenye matawi yaliyo tanda.
 
49Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
 
50Ndani yake zimo chemchem mbili zinazo pita.
 
51Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
 
52Humo katika kila matunda zimo namna mbili.
 
53Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
 
54Wawe wameegemea matandiko yenye bit'ana ya hariri nzito; na matunda ya Bustani hizo yapo karibu.
 
55Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
 
56Humo watakuwamo wanawake watulizao macho yao; hajawagusa mtu kabla yao wala jini.
 
57Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
 
58Kama kwamba wao ni yakuti na marijani.
 
59Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha.
 
60Ati yaweza kuwa malipo ya ihsani ila ihsani?
 
61Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
 
62Na zaidi ya hizo zipo Bustani nyengine mbili.
 
63Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
 
64Za kijani kibivu.
 
65Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
 
66Na chemchem mbili zinazo furika.
 
67Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
 
68Imo humo miti ya matunda, na mitende na mikomamanga.
 
69Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
 
70Humo wamo wanawake wema wazuri.
 
71Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
 
72Wanawake wazuri wanao tawishwa katika makhema.
 
73Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
 
74Hajawagusa mtu wala jini kabla yao.
 
75Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
 
76Wameegemea juu ya matakia ya kijani na mazulia mazuri.
 
77Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
 
78Limetukuka jina la Mola wako Mlezi Mwenye utukufu na ukarimu.