___Translations___

_Quran?_

_Gadgets_

_Search_

_Links_

_Contribute_

_Note_

1 - AL-FAATIH'A
2 - AL - BAQARA
3 - AL I'MRAN
4 - AN-NISAAI
5 - AL - MAIDA
6 - AL - AN-A'AM
7 - AL - A'RAAF
8 - AL - ANFAAL
9 - AT-TAWBA
10 - YUNUS
11 - HUD
12 - YUSUF
13 - AR-RAA'D
14 - IBRAHIM
15 - AL - HIJR
16 - AN NAH'L
17 - AL ISRAAI (BANI ISRAIL)
18 - AL - KAHF
19 - MARYAM
20 - T'AHA
21 - AL - ANBIYAA
22 - AL -HAJJ
23 - AL - MUUMINUN
24 - AN - NUR
25 - AL - FURQAN
26 - ASH-SHUA'RAA
27 - AN-NAML
28 - AL-QAS'AS'
29 - AL - A'NKABUT
30 - AR-RUM
31 - LUQMAN
32 - ASSAJDAH
33 - AL-AH'ZAB
34 - SABAA
35 - FAAT'IR
36 - YA-SIN
37 - ASS'AFFAT
38 - S'AAD
39 - AZZUMAR
40 - GHAAFIR (AU AL MUUMIN)
41 - FUSS'ILAT (AU H'A MIM SAJDAH)
42 - ASH-SHUURA
43 - AZZUKHRUF
44 - ADDUKHAN
45 - AL - JAATHIYA
46 - AL - AH'QAAF
47 - MUH'AMMAD
48 - AL FAT-H'I
49 - AL H'UJURAAT
50 - QAAF
51 - ADH-DHAARIYAAT
52 - ATT'UR
53 - ANNAJM
54 - AL-QAMAR
55 - ARRAH'MAN
56 - AL -WAAQIA'H
57 - AL -H'ADIID
58 - AL - MUJAADALAH
59 - AL - H'ASHRI
60 - AL - MUMTAH'INAH
61 - ASS'AF
62 - AL - JUMUA'
63 - AL - MUNAAFIQUN
64 - ATTAGHAABUN
65 - ATT'ALAAQ
66 - ATTAH'RIIM
67 - AL - MULK
68 - AL - QALAM
69 - AL - H'AAQQAH
70 - AL - MAA'RIJ
71 - NUH'
72 - AL - JINN
73 - AL - MUZZAMMIL
74 - AL - MUDDATHTHIR
75 - AL - QIYAMAH
76 - AL - INSAN
77 - AL - MURSALAAT
78 - ANNABAA
79 - ANNAZIA'AT
80 - A'BASA
81 - ATTAKWIR
82 - AL - INFIT'AAR
83 - AL - MUT'AFFIFIIN
84 - AL - INSHIQAAQ
85 - AL - BURUUJ
86 - ATT'AARIQ
87 - AL - AA'LAA
88 - AL - GHAASHIYAH
89 - AL - FAJR
90 - AL - BALAD
91 - ASH-SHAMS
92 - AL - LAYL
93 - WADH-DHUH'AA
94 - ASH-SHARH'
95 - AT-TIN
96 - AL - A'LAQ
97 - AL - QADR
98 - AL - BAYYINAH
99 - AZ-ZILZALAH
100 - AL - A'ADIYAAT
101 - AL - QAARIA'H
102 - AT-TAKAATHUR
103 - AL - A'S'R
104 - AL - HUMAZAH
105 - AL - FIIL
106 - QURAISH
107 - AL - MAAU'N
108 - AL - KAWTHAR
109 - AL - KAFIRUN
110 - ANNAS'R
111 - AL - MASAD
112 - AL - IKHLAS'
113 - AL - FALAQ
114 - ANNAS
KISWAHILI

79 - ANNAZIA'AT

 

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.

 
1Naapa kwa wanao komoa kwa nguvu,
 
2Na kwa wanao toa kwa upole,
 
3Na wanao ogelea,
 
4Wakishindana mbio,
 
5Wakidabiri mambo.
 
6Siku kitapo tetemeka cha kutetemeka,
 
7Kifuate cha kufuatia.
 
8Siku hiyo nyoyo zitapiga piga,
 
9Macho yatainama chini.
 
10Sasa wanasema: Ati kweli tutarudishwa kwenye hali ya kwanza?
 
11Hata tukiwa mifupa iliyo bunguliwa?
 
12Wanasema: Basi marejeo hayo ni yenye khasara!
 
13Kwa hakika hayo ni ukelele mmoja tu,
 
14Mara watakuwa kwenye uwanda wa mkutano!
 
15Je! Imekufikia hadithi ya Musa?
 
16Mola wake Mlezi alipo mwita katika bonde takatifu la T'uwaa, akamwambia:
 
17Nenda kwa Firauni. Hakika yeye amezidi jeuri.
 
18Umwambie: Je! Unapenda kujitakasa?
 
19Nami nitakuongoa ufike kwa Mola wako Mlezi, upate kumcha.
 
20Basi alimwonyesha Ishara kubwa.
 
21Lakini aliikadhibisha na akaasi.
 
22Kisha alirudi nyuma, akaingia kufanya juhudi.
 
23Akakusanya watu akanadi.
 
24Akasema: Mimi ndiye Mola wenu Mlezi mkuu kabisa.
 
25Basi hapo Mwenyezi Mungu akamshika kumuadhibu kwa la mwisho na la mwanzo.
 
26Kwa hakika katika haya yapo mazingatio kwa wanao ogopa.
 
27Je! Ni vigumu zaidi kukuumbeni nyinyi au mbingu? Yeye ndiye aliye ijenga!
 
28Akainua kimo chake, na akaitengeneza vizuri.
 
29Na akautia giza usiku wake, na akautokeza mchana wake.
 
30Na juu ya hivyo ameitandaza ardhi.
 
31Akatoa ndani yake maji yake na malisho yake,
 
32Na milima akaisimamisha,
 
33Kwa nafuu yenu na mifugo yenu.
 
34Basi itakapo fika hiyo balaa kubwa,
 
35Siku ambayo mtu atakumbuka aliyo yafanya,
 
36Na Jahannamu itadhihirishwa kwa mwenye kuona,
 
37Basi ama yule aliye zidi ujeuri,
 
38Na akakhiari maisha ya dunia,
 
39Kwa hakika Jahannamu ndiyo makaazi yake!
 
40Na ama yule anaye ogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi, na akajizuilia nafsi yake na matamanio,
 
41Basi huyo, Pepo itakuwa ndiyo makaazi yake!
 
42Wanakuuliza Saa (ya Kiyama) itakuwa lini?
 
43Una nini wewe hata uitaje?
 
44Kwa Mola wako Mlezi ndio mwisho wake.
 
45Kwa hakika wewe ni mwonyaji tu kwa mwenye kuikhofu.
 
46Ni kama kwamba wao siku watapo iona (hiyo Saa) hawakukaa ila jioni moja tu, au mchana wake.