Translations Suras
KISWAHILI

111 - AL - MASAD

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.

 
1Imeangamia mikono ya Abu Lahab, na yeye pia ameangamia.
 
2Hayatamfaa mali yake, wala alivyo vichuma.
 
3Atauingia Moto wenye mwako.
 
4Na mkewe, mchukuzi wa kuni,
 
5Shingoni mwake iko kamba iliyo sokotwa.
 
 
ReadTheQuran.org