Translations Suras
KISWAHILI

104 - AL - HUMAZAH

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.

 
1Ole wake kila safihi, msengenyaji!
 
2Aliye kusanya mali na kuyahisabu.
 
3Anadhani ya kuwa mali yake yatambakisha milele!
 
4Hasha! Atavurumishwa katika H'ut'ama.
 
5Na nani atakujuvya ni nini H'ut'ama?
 
6Moto wa Mwenyezi Mungu ulio washwa.
 
7Ambao unapanda nyoyoni.
 
8Hakika huo utafungiwa nao
 
9Kwenye nguzo zilio nyooshwa.
 
 
ReadTheQuran.org