Translations Suras
KISWAHILI

101 - AL - QAARIA'H

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.

 
1Inayo gonga!
 
2Nini Inayo gonga?
 
3Na nini kitacho kujuilisha nini Inayo gonga?
 
4Siku ambayo watu watakuwa kama nondo walio tawanyika;
 
5Na milima itakuwa kama sufi zilizo chambuliwa!
 
6Basi yule ambaye mizani yake itakuwa nzito,
 
7Huyo atakuwa katika maisha ya kupendeza.
 
8Na yule ambaye mizani yake itakuwa khafifu,
 
9Huyo maskani yake yatakuwa Moto wa Hawiya!
 
10Na nini kitacho kujuilisha nini hiyo?
 
11Ni Moto mkali!
 
 
ReadTheQuran.org