Translations Suras
KISWAHILI

99 - AZ-ZILZALAH

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.

 
1Itakapo tetemeshwa ardhi kwa mtetemeko wake!
 
2Na itakapo toa ardhi mizigo yake!
 
3Na mtu akasema: Ina nini?
 
4Siku hiyo itahadithia khabari zake.
 
5Kwa sababu Mola wake Mlezi ameifunulia!
 
6Siku hiyo watu watatoka kwa mfarakano wakaonyweshwe vitendo vyao!
 
7Basi anaye tenda chembe ya wema, atauona!
 
8Na anaye tenda chembe ya uovu atauona!
 
 
ReadTheQuran.org