Translations Suras
KISWAHILI

96 - AL - A'LAQ

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.

 
1Soma kwa jina la Mola wako Mlezi aliye umba,
 
2Amemuumba binaadamu kwa tone la damu,
 
3Soma! Na Mola wako Mlezi ni Karimu kushinda wote!
 
4Ambaye amefundisha kwa kalamu.
 
5Kamfundisha mtu aliyo kuwa hayajui.
 
6Kwani! Hakika mtu bila ya shaka huwa jeuri
 
7Akijiona katajirika.
 
8Hakika kwa Mola wako Mlezi ndio marejeo.
 
9Umemwona yule anaye mkataza
 
10Mja anapo sali?
 
11Umeona kama yeye yuko juu ya uwongofu?
 
12Au anaamrisha uchamngu?
 
13Umeona kama yeye akikanusha na anarudi nyuma?
 
14Hajui ya kwamba Mwenyezi Mungu anaona?
 
15Kwani! Kama haachi, tutamkokota kwa shungi la nywele!
 
16Shungi la uwongo, lenye makosa!
 
17Basi na awaite wenzake!
 
18Nasi tutawaita Mazabania!
 
19Hasha! Usimt'ii! Nawe sujudu na ujongee!
 
 
ReadTheQuran.org