Translations Suras
KISWAHILI

93 - WADH-DHUH'AA

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.

 
1Naapa kwa mchana!
 
2Na kwa usiku unapo tanda!
 
3Mola wako Mlezi hakukuacha, wala hakukasirika nawe.
 
4Na bila ya shaka wakati ujao utakuwa bora kwako kuliko ulio tangulia.
 
5Na Mola wako Mlezi atakupa mpaka uridhike.
 
6Kwani hakukukuta yatima akakupa makaazi?
 
7Na akakukuta umepotea akakuongoa?
 
8Akakukuta mhitaji akakutosheleza?
 
9Basi yatima usimwonee!
 
10Na anaye omba au kuuliza usimkaripie!
 
11Na neema za Mola wako Mlezi zisimlie.
 
 
ReadTheQuran.org