Translations Suras
KISWAHILI

92 - AL - LAYL

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.

 
1Naapa kwa usiku unapo funika!
 
2Na mchana unapo dhihiri!
 
3Na kwa Aliye umba dume na jike!
 
4Hakika juhudi zenu bila ya shaka ni mbali mbali.
 
5Ama mwenye kutoa na akamchamngu,
 
6Na akaliwafiki lilio jema,
 
7Tutamsahilishia yawe mepesi.
 
8Na ama mwenye kufanya ubakhili, na asiwe na haja ya wenzake,
 
9Na akakanusha lilio jema,
 
10Tutamsahilishia yawe mazito!
 
11Na mali yake yatamfaa nini atapo kuwa anadidimia?
 
12Hakika ni juu yetu kuonyesha uwongofu.
 
13Na hakika ni yetu Sisi Akhera na dunia.
 
14Basi nakuonyeni na Moto unao waka!
 
15Hatauingia ila mwovu kabisa!
 
16Anaye kadhibisha na kupa mgongo.
 
17Na mchamngu ataepushwa nao,
 
18Ambaye hutoa mali yake kwa ajili ya kujitakasa.
 
19Na wala si kwa kuwa yupo yeyote aliye mfanyia hisani ndio anamlipa.
 
20Ila ni kutaka radhi ya Mola wake Mlezi aliye juu kabisa.
 
21Naye atakuja ridhika!
 
 
ReadTheQuran.org