Translations Suras
KISWAHILI

89 - AL - FAJR

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.

 
1Naapa kwa alfajiri,
 
2Na kwa masiku kumi,
 
3Na kwa viwili viwili na kimoja kimoja,
 
4Na kwa usiku unapo pita,
 
5Je! Hapana katika haya kiapo kwa mwenye akili?
 
6Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo wafanya kina A'di?
 
7Wa Iram, wenye majumba marefu?
 
8Ambao haukuumbwa mfano wake katika nchi?
 
9Na Thamudi walio chonga majabali huko bondeni?
 
10Na Firauni mwenye vigingi?
 
11Ambao walifanya jeuri katika nchi?
 
12Wakakithirisha humo ufisadi?
 
13Basi Mola wako Mlezi aliwapiga mjeledi wa adhabu.
 
14Hakika Mola wako Mlezi yupo kwenye mavizio anawavizia.
 
15Ama mtu anapo jaribiwa na Mola wake Mlezi, akamkirimu na akamneemesha, husema: Mola wangu Mlezi amenikirimu!
 
16Na ama anapo mjaribu akampunguzia riziki yake, husema: Mola wangu Mlezi amenitia unyonge!
 
17Sivyo hivyo! Bali nyinyi hamuwakirimu mayatima,
 
18Wala hamhimizani kulisha masikini;
 
19Na mnakula urithi kwa ulaji wa pupa,
 
20Na mnapenda mali pendo la kupita kiasi.
 
21Sivyo hivyo! Itakapo vunjwa ardhi vipande vipande,
 
22Na akaja Mola wako Mlezi na Malaika safu safu,
 
23Na ikaletwa Jahannamu siku hiyo, siku hiyo mtu atakumbuka! Lakini kukumbuka huko kutamfaa nini?
 
24Atasema: Laiti ningeli jitangulizia kwa uhai wangu!
 
25Basi siku hiyo hataadhibu yeyote namna ya kuadhibu kwake.
 
26Wala hatafunga yeyote kama kufunga kwake.
 
27Ewe nafsi iliyo tua!
 
28Rejea kwa Mola wako Mlezi umeridhika, na umemridhisha.
 
29Basi ingia miongoni mwa waja wangu,
 
30Na ingia katika Pepo yangu.
 
 
ReadTheQuran.org