Translations Suras
KISWAHILI

86 - ATT'AARIQ

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.

 
1Naapa kwa mbingu na Kinacho kuja usiku!
 
2Na nini kitakacho kujuulisha ni nini hicho Kinacho kuja usiku?
 
3Ni Nyota yenye mwanga mkali.
 
4Hapana nafsi ila inayo mwangalizi.
 
5Hebu naajitazame mwanaadamu ameumbwa kwa kitu gani?
 
6Ameumbwa kwa maji yatokayo kwa kuchupa,
 
7Yatokayo baina ya mifupa ya mgongo na mbavu.
 
8Hakika Yeye ana uweza wa kumrudisha.
 
9Siku zitakapo dhihirishwa siri.
 
10Basi hatakuwa na nguvu wala msaidizi.
 
11Naapa kwa mbingu yenye marejeo!
 
12Na kwa ardhi inayo pasuka!
 
13Hakika hii ni kauli ya kupambanua.
 
14Wala si mzaha.
 
15Hakika wao wanapanga mpango.
 
16Na Mimi napanga mpango.
 
17Basi wape muhula makafiri - wape muhula pole pole.
 
 
ReadTheQuran.org