Translations Suras
KISWAHILI

85 - AL - BURUUJ

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.

 
1Naapa kwa mbingu yenye Buruji!
 
2Na kwa siku iliyo ahidiwa!
 
3Na kwa shahidi na kinacho shuhudiwa!
 
4Wameangamizwa watu wa makhandaki
 
5Yenye moto wenye kuni nyingi,
 
6Walipo kuwa wamekaa hapo,
 
7Na wao ni mashahidi wa yale waliyo kuwa wakiwafanyia Waumini.
 
8Nao hawakuona baya lolote kwao ila kuwa wakimuamini Mwenyezi Mungu, Mwenye nguvu, Msifiwa,
 
9Ambaye anao ufalme wa mbingu na ardhi; na Mwenyezi Mungu ni shaahidi wa kila kitu.
 
10Hakika walio wafitini Waumini wanaume na Waumini wanawake, kisha hawakutubu, basi watapata adhabu ya Jahannamu na watapata adhabu ya kuungua.
 
11Hakika walio amini na wakatenda mema watapata Bustani zenye mito ipitayo kati yake. Huko ndiko kufuzu kukubwa.
 
12Hakika kutesa kwa Mola wako Mlezi ni kukali.
 
13Yeye ndiye anaye anzisha na ndiye anaye rejeza tena,
 
14Naye ni Mwenye kusamehe, Mwenye mapenzi,
 
15Mwenye Kiti cha Enzi, Mtukufu,
 
16Atendaye ayatakayo.
 
17Je! Zimekuwasilia khabari za majeshi?
 
18Ya Firauni na Thamudi?
 
19Lakini walio kufuru wamo katika kukadhibisha.
 
20Na Mwenyezi Mungu nyuma yao amewazunguka.
 
21Bali hii ni Qur'ani tukufu
 
22Katika Ubao Ulio Hifadhiwa.
 
 
ReadTheQuran.org