Translations Suras
KISWAHILI

84 - AL - INSHIQAAQ

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.

 
1Itapo chanika mbingu,
 
2Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza,
 
3Na ardhi itakapo tanuliwa,
 
4Na kuvitoa vilivyo kuwa ndani yake, ikawa tupu,
 
5Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza,
 
6Ewe mtu! Hakika wewe unajikusuru kwa juhudi kumwendea Mola wako Mlezi, basi utamkuta.
 
7Ama atakaye pewa daftari lake kwa mkono wa kulia,
 
8Basi huyo atahisabiwa hisabu nyepesi,
 
9Na arudi kwa ahali zake na furaha.
 
10Na ama atakaye pewa daftari lake kwa nyuma ya mgongo wake,
 
11Basi huyo ataomba kuteketea.
 
12Na ataingia Motoni.
 
13Hakika alikuwa furahani kati ya jamaa zake.
 
14Huyo hakika alidhani kuwa hatarejea tena.
 
15Kwani? Hakika Mola wake Mlezi alikuwa akimwona!
 
16Basi ninaapa kwa wekundu wa jua linapo kuchwa,
 
17Na kwa usiku na unavyo vikusanya,
 
18Na kwa mwezi unapo pevuka,
 
19Lazima mtapanda t'abaka kwa t'abaka!
 
20Basi wana nini hawaamini?
 
21Na wanapo somewa Qur'ani hawasujudu?
 
22Bali walio kufuru wanakanusha tu.
 
23Na Mwenyezi Mungu anajua wanayo yadhamiria.
 
24Basi wabashirie adhabu chungu!
 
25Isipo kuwa wale walio amini na wakatenda mema; hao watakuwa na ujira usio malizika.
 
 
ReadTheQuran.org