Translations Suras
KISWAHILI

82 - AL - INFIT'AAR

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.

 
1Mbingu itapo chanika,
 
2Na nyota zitapo tawanyika,
 
3Na bahari zitakapo pasuliwa,
 
4Na makaburi yatapo fukuliwa,
 
5Hapo kila nafsi itajua ilicho tanguliza, na ilicho bakisha nyuma.
 
6Ewe mwanaadamu! Nini kilicho kughuri ukamwacha Mola wako Mlezi Mtukufu?
 
7Aliye kuumba, akakuweka sawa, akakunyoosha,
 
8Katika sura yoyote aliyo ipenda akakujenga.
 
9Sivyo hivyo! Bali nyinyi mnaikanusha Siku ya Malipo.
 
10Na hakika bila ya shaka wapo walinzi juu yenu,
 
11Waandishi wenye hishima,
 
12Wanayajua mnayo yatenda.
 
13Hakika wema bila ya shaka watakuwa katika neema,
 
14Na hakika waovu bila ya shaka watakuwa Motoni;
 
15Wataingia humo Siku ya Malipo.
 
16Na hawatoacha kuwamo humo.
 
17Na nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?
 
18Tena nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?
 
19Siku ambayo nafsi haitakuwa na madaraka yoyote juu ya nafsi; na amri yote siku hiyo ni ya Mwenyezi Mungu tu.
 
 
ReadTheQuran.org