Translations Suras
KISWAHILI

81 - ATTAKWIR

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.

 
1Jua litakapo kunjwa, s
 
2Na nyota zikazimwa,
 
3Na milima ikaondolewa,
 
4Na ngamia wenye mimba pevu watakapo achwa wasishughulikiwe,
 
5Na wanyama wa mwituni wakakusanywa,
 
6Na bahari zikawaka moto,
 
7Na nafsi zikaunganishwa,
 
8Na msichana aliye zikwa hai atapo ulizwa,
 
9Kwa kosa gani aliuliwa?
 
10Na madaftari yatakapo enezwa,
 
11Na mbingu itapo tanduliwa,
 
12Na Jahannamu itapo chochewa,
 
13Na Pepo ikasogezwa,
 
14Kila nafsi itajua ilicho kihudhurisha.
 
15Naapa kwa nyota zinapo rejea nyuma,
 
16Zinazo kwenda, kisha zikajificha,
 
17Na kwa usiku unapo pungua,
 
18Na kwa asubuhi inapo pambazuka,
 
19Kwamba hakika bila ya shaka hii ni kauli ya Mjumbe mtukufu,
 
20Mwenye nguvu na mwenye cheo kwa huyo Mwenye Kiti cha Enzi,
 
21Anaye t'iiwa, tena muaminifu.
 
22Na wala huyu mwenzenu hana wazimu.
 
23Na hakika yeye alimwona kwenye upeo wa macho ulio safi.
 
24Wala yeye si bakhili kwa mambo ya ghaibu.
 
25Wala hii si kauli ya Shetani maluuni.
 
26Basi mnakwenda wapi?
 
27Haikuwa hii ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.
 
28Kwa yule miongoni mwenu anaye taka kwenda sawa.
 
29Wala nyinyi hamtataka isipo kuwa atake Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote.
 
 
ReadTheQuran.org